WANANCHI WASOTA VILIO VYATALA KUTOKUKUTA MAJINA YAO KWENYE VITUO VYA KUPIGIA KURA WAAMUA KUWEKA KAMBI HADI KIELEWEKE.
🔻NADO NA MURIET MASHARIKI NGOMA BADO MBICHI MASANDUKU YA KUPIGIA KURA KUCHELEWA.
Na Lucas Myovela - Arusha.
Hali hii imetufanya tuweze kumtafuta Msimamizi wa uchaguzi ngazi ya wilaya John Kayombo ambeye ndiye Mkurugenzi wa jiji la Arusha na kueleza kuwa vyama 12 viliweza kuchukua fomu za mawakala na wasimamizi wao na kula kiapo isipokuwa chadema peke yake ndiyo kulikuwa na mvutano.
"Chadema waliweka mawakala wengi sana unakuta kituo kimoja mawakala 5 au 3 kitu ambacho ni kinyume na utaratibu na tuliwaita waje wapunguze baadhi ya mawakala na wabaki wale wanao hitajika lakini hadi jana jioni walikuwa bado wanamvutano na hakuna hadi sasa waliyokula kiapo". Ameongeza Kayombo.
"Kwasasa Vijana wanajitambua na wanajua thamani ya kiongozi na haya yote yalitokanana na utoaji wa elimu kwa vijana na wananchi kwa ujumla". Amesema Said
"Kuhusu mawakala nahisi vyama vya upinzani walikuwa hawajajipanga maana hata katika hatua ya uandikishaji hawakuweka mawakala ndiyo maana naona hiyo hali hadi sasa, Katika kata ya unga ltd kuna vituo 18 vya kupiga kura na kila mtaa kuna vituo 3 na tunayo mitaa sita, na hii inatokana na kuwa na watu wengi na kwa kasi hii ninaimani uchaguzi utaisha salama". Ameongeza Said.
Aidha Sakata la kutokua na mawakala inaelezwa kuwa jana majira ya usiku mgombea wa chadema mtaa wa Viwandani alijitoa katika nafasi hiyo ya kugombea na kujiunga na chama cha mapinduzi (CCM).
Wakiongea na Motive Media wameeleza kuwa walijitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari katika kituo hicho cha Logdong kata ya Sokoni one lakini cha kushangaza leo majina hayapo na majina waliyo yakuta ni yawatu wengine kabisa.
Hata hivyo katika kituo cha Engasengiu kata ya Sinoni, Mmoja ya wagombea wa nafasi ya mwenyekiti Damiano Mollel (CHADEMA) amejikuta akiangua kilio baada ya kukosa jina lake kwenye kituo cha kura kitu ambacho anasema ni hujuma kubwa zimefanyika.
Na Katika Mtaa wa Muriet mashariki katika kata hiyo hiyo ya Muriet hadi masanduku ya kupigia kura yamefika majira ya saa 09:30 Asubuhi.
Hali hii imetufanya tumtafute diwani ya kata hiyo ya Muriet Frances Mbise na ameweza kukiri kuwepo kwa changamoto hizo na kueleza kuwa anaendelea na jitihada za kumtafuta msimamizi wa uchaguzi ili aweze kujua tatizo lipo wapi.
"Wananchi wengi watakosa nafasi zao za msingi za kumchagua kiongozi wanao mtaka kutokana na hali hii ya kuwa na jua kali na majina ya wananchi yengi kutokuonekana katika makaratasi yaliyo bandikwa". Amesema.
"Wasimamizi wangewapa wananchi nafasi ya kutaja majina yao na wakaangalia katika daftari za kuhakiki walizo nazo, kwa kuwanyima fursa wanchi ni kuwanyima haki yao ya kikatiba, niwaombe wanao husika kujaribu kuangalia upya namna ya kuwasaidia wananchi wanateseka sana wanapokuta ugumu wa majina yao hayapo". Amesema.
Comments
Post a Comment