YATOA MIKOPO YA TRILIONI 10.9 KATIKA SEKTA ZOTE KUUNGA JUHIDI ZA RAIS DKT. SAMIA KUBORESHA MAISHA YA WANANCHI.
Na Lucas Myovela - Arusha.
Mkude ameeleza kuwa Taasisi za fedha mfano Benki ya CRDB ambayo ni kampuni mama ya CRDB Bank Foundation ni miongoni mwa sehemu za uhakika kupata elimu ya fedha ya kufanikisha mipango ya watanzania.
"Uwepo wa Taasisi ya CRDB Bank Foundation hapa Arusha leo ni fursa kwa wanawake na vijana wetu kuelimika na kuanza kufanya biashara kwa malengo makubwa yatakayosaidia kukuza kipato cha mtu binafsi, uchumi wa kaya na taifa kwa ujumla.
Aidha Mkunde amewataka watanzania wote kutumia fursa hiyo na kuhakikisha wanaendeleza uhusiano huo kwa ushauri na mafunzo ya ujasiriamali kutoka kwa wataalamu wa fedha kutoka VRDB BANK maana ni nyenzo muhimu ya kukuza biashara.
Pia Mkude ameeleza kuwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inashirikiana na sekta binafsi kuwafikia wananchi popote walipo kuanzia vijijini mpaka mjini na kuwataka watanzania kuhakikisha wanatumia kila fursa inayolingana na uwezo wao ili kukuza uchumi binafsi bila kukurupuka.
Rabella ameongeza kuwa hadi mwishoni mwa mwezi Machi 2025, Benki ya CRDB ilikuwa imetoa jumla ya mikopo ya shilingi trillion 10.946 kwa sekta zote na zaidi ya asilimia 30 ya mikopo hiyo ilielekezwa kwa wajasiriamali wadogo na wa kati.

"Programu ya IMBEJU imejikita katika kupeleka uwezeshaji kwa wajasiriamali wa sekta zote za uchumi ikiwemo biashara, kilimo, ufugaji, uzalishaji na ubunifu wa kiteknolojia kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kitaifa na kimataifa, tunapanua wigo wa fursa na kuhakikisha huduma zetu zinawafikia walengwa kote nchini". Ameongea Rabella.
Aidha Rabella ameongeza kuwa ili kunufaika na fursa za mitaji wezeshi wanayotoa kwa mjasiriamali aliye kwenye kikundi anatakiwa kuhudhuria mafunzo na kuwa na biashara maana kuwepo kwake kwenye kikundi ni kinga ya kutotakiwa kuwasilisha dhamana akihitaji mtaji wezeshi kuanzia shilingi laki mnili (200,000) mpaka shilingi milioni kumi (10,000,000).
Comments
Post a Comment