KISHINDO CHA KARIBU KILIFAIR 2025 NCHI ZAIDI YA 40 KUSHIRIKI,WADAU WA UTALII ZAIDI YA 800 KUWEKA KAMBI ARUSHA

🔻IJUE HOTELI YA KITALII YA KIBO PALACE ARUSHA YENYE CHUMBA CHA TOFAUTI CHA KULALA RAIS YEYOTE DUNIANI.

Na Lucas Myovela -Arusha.

Maonesho kubwa la utalii duniani la KARIBU KILIFAIR yanayofanyika Afrika ya Mashariki nchini Tanzania kwa mwaka huu wa 2025 yanatazamiwa kuwa tofauti na miaka mingine ambapo kwasasa inatazamiwa kuwakusanya kwa pamoja wadau zaidi 800 katika sekta ya utalii duniani kote kuanzia Juni 6 hadi 8 2025, yakiwakutanisha wadau wa utalii kutoka sehemu mbalimbali duniani ili kuionyesha Tanzania kama kivutio kikuu cha burudani na biashara.Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi Mkuu wa KiliFair Promotions, Dominic Shoo, alielezea Karibu-KiliFair (KKF) kama maonyesho ya utalii ya Afrika Mashariki, yaliyotokana na kuunganishwa kwa maonyesho mawili makubwa ya utalii nchini Tanzania.


"Tukio la mwaka huu linatarajiwa kukaribisha waonyeshaji zaidi ya 500 kutoka nchi 13, zaidi ya mawakala 800 wa usafiri waliosajiliwa kutoka nchi 40+ na kuvutia takriban watalii 15,000 na wapenda usafiri, Karibu-KiliFair kwa mara nyingine tena ni maonyesho makubwa zaidi na muhimu ya utalii katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara,"Ameeleza Shoo.


"Kaulimbiu yetu, 'Pale Biashara Inapokutana na Wanyamapori', inaendelea kututofautisha duniani kote. Tanzania imesalia kuwa kivutio cha juu cha PANYA (Mikutano, Motisha, Mikutano na Maonesho), mojawapo ya maeneo machache ambapo matukio ya biashara yanachanganyikana na uzoefu wa ajabu wa wanyamapori". Ameongeza Shoo.Aidha Shoo aliongeza kuwa maonesho hayo yatakuwa na manufaa makubwa kwa washiriki kujifunza na kujionea vivutio mbalimbali hapa nchini ili waweze kuwa mabalozi wazuri wa kuleta watalii nchini kutoka mataifa mbalimbali duniani ambapo mpaka sasa kampuni yake imefanikiwa kupitia matamasha mbalimbali na kuwakutanisha wadau wa utalii wa hapa nchini na nchi za ulaya lengo likiwa ni kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo hapa nchini Kimataifa.


Mkurugenzi Mwenza wa KARIBU KILIFAIR, Tom Kunkler, aliipongeza Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuipa kipaumbele sekta ya utalii kwa kuendeleza vivutio vipya, hifadhi za taifa na motisha kwa wawekezaji.


Alisema Tanzania inasalia kuwa kivutio kinachotambulika duniani kwa utalii wa asili, sehemu ya soko lenye ushindani mkubwa katika Afrika Mashariki. 

KIBO PALACE HOTEL ni miongoni mwa wadhani wa maonyesho hayo makubwa ya utalii ya KARIBU KILIFAIR ambapo meneja wa Hotel hiyo Ndg. Hashim Mohamed alisema kuwa uongozi wa hoteli hiyo pamoja na watumishi wapo tayari wakati wote kuwapokea wageni kutoka kila kona ya ulimwengu na kuwapa huduma bora hata kama ni kiongozi wa nchi maana vipo vyumba maalumu kwaajili ya wakuu wa nchi.

Bi. Beatrice Laswai ni mmoja ya wakurugenzi katika Hoteli hiyo ya kifahari ya kitalii ya KIBO PALACE HOTEL ambapo anaeleza kuwa hoteli hiyo ni moja ya hoteli kongongwe na pendwa kwa watalii hata kwa watanzania kutokana na ubora wa huduma zao kitu ambacho kinaifanya hoteli hiyo kuendelea kuongoza kuwa hoteli yenye hadhi ya nyota tano miongoni mwa hoteli chache zenye hadhi hiyo nchini Tanzania.

"Sisi kama wadhamini tutakuwepo katika maonyesho haya makubwa ya utalii na tutakuwa na banda letu la maonesho ambalo litatambulisha huduma zote zinazopatikana katika hoteli ya KIBO PALACE na wale watakaokosa huduma zetu hapa Arusha tuna hoteli nyingine Moshi Mkoani Kilimanjaro".Amesema Bi. Laswai.





Akiwakilisha Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), Afisa Mkuu wa Uhifadhi - Utalii, Bi Eunice Msangi, aliipongeza KiliFair Promotions kwa dhamira yake ya kukuza sekta ya utalii Tanzania.


"Tunawakaribisha wadau na wananchi wote kuhudhuria Karibu-KiliFair 2025 ili kujifunza zaidi kuhusu uhifadhi na utalii. TANAPA itakuwepo ili kuonyesha hifadhi zetu za taifa, kubadilishana fursa za uwekezaji na kutoa taarifa za kina kuhusu maeneo yote ya hifadhi," alisema.


Akizungumza kwa niaba ya Benki ya CRDB, Meneja wa Biashara wa Kanda ya Kaskazini, Emmanuel Kafui, alisisitiza uungaji mkono wa benki hiyo kwa sekta ya utalii.


"Wakati utalii unavyoendelea kukua kwa kasi, Benki ya CRDB imejitolea kusaidia wateja katika sekta hii ya utalii," alisema.

"Tunatoa mikopo ya mahema kwa ajili ya huduma za malazi kuanzia 1m/- hadi 500m/-, bila dhamana inayohitajika."


Comments