MAAFISA AFYA WAWILI WA JIJI LA ARUSHA JELA MIAKA MITATU AU KULIPA FAINI KALI.

đź’˘WAKUTWA NA HATIA KWA KOSA LA KUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA NZITO KUTOKA KWA KIGOGO WA KIWANDA.

Na Lucas Myovela - Arusha.

Katika utendaji wa kazi katika hatua za kupambana na vitendo vya rushwa hapa nchini, Kupitia Taasisi ya Kupambana na rushwa Mkoa wa Arusha umeweza kuwakamata watumishi wawili wa sekta ya Afya kata ya Terati katika Halmashauri ya Jiji la Arusha.


Katika hatua hiyo Takukuru Mkoa wa Arusha mnamo Julai 18, 2025 iliweza kufungua shauri la jinai namba. 17569/2025 dhidi ya Maafisa Afya hao ambao mshtakiwa wa kwanza ni Dickson Chinyuka Ndumbalo na mshitakiwa wa pili ni Keneth Tamzi Twinzi, ambapo wote wapatindishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arusha.

Shauri hilo lilikuwa likisikizwa nambele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Mhe. Regina Oiyer, na kuongozwa na kuendeshwa na Jopo la mawakili wawili wa serikali, Wakilimsomi Melvin Richard na wakili Msomi Halima Saidi.


Katika Shitaka hilo washtakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na kosa la kuomba na kupokea rushwa kinyume na kifungu cha 15(1)(a),(2) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura 329 Marejeo ya Mwaka 2023.


Maafisa hao wa serikali sekta ya Afya waliomba na kupokea rushwa Kiasi cha Shilingi Milioni Moja (1,000,000/=) kutoka kwa Meneja wa kiwanda cha Mbunumbundi kwa lengo la kutokumchukulia hatua za kisheria kwa kosa la uchakavu wa magari ya kiwanda hicho.


Baada ya kusomewa hati ya mashtaka hayo mnano tarehe 18/5/2025, washtakiwa walikana makosa yao na shauri lilisikilizwa kwa kipindi cha mwaka mmoja ikwa ninpamoja na utoaji wa ushahidi kwa kadili ya muongozo wa usikilizwaji wa kesi.


Akisoma Hukumu hiyo baada ya kesi hiyo kusikilizwa kwa pande zote mbili Mnamo tarehe 28.05.2026 mbele ya hakimu mkazi wa mahakama hiyo Mhe. Regina Oiyer, na mahakama iliwakuta na hatia washtakiwa wote wawili kwa makosa mawili ya kuomba na kupokea rushwa.


Aidha Baada ya Mahakama kuwakuta na hatia iliweza kuwahukumu kwenda jela miaka mitatu au kilipa faini ya shilingi Laki tano kwa kila kosa moja, washtakiwa waliweza kulipa faini hiyo iliyotolewa na mahakama.

Akitoa Taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Arusha Zawadi Ngailo, ameeleza kuwa Takukuru imeweza kushinda keshi hiyo namba CC 17569/2025 na kueleza kuwa bado wapo macho na wataendelea kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha vitendo vya rushwa vinatokemezwa na wanachi kupata huduma kwa mujibu wa sheria za nchi.


Aidha Ngailo amewataka wananchi wote kuendelea kutoa taarifa zozote zenye viashiria vya rushwa kwa mqmlqka husika na kuhakikisha pindi watuhumiwa wanapo kamatwa na kufikishwa mahakamani wafike kutoa ushahidi.

Comments