ATAKA WATOTO WASIYO NA SARE KUENDELEA NA MASOMO.
Na Lucas Myovela_Simanjiro.
Zoezi hilo la ugawaji wa vyakula mashuleni limelatiba na shirika la maendeleo la Eclat Foundation lililopo wilayani Simanjiro Mkoani Manyara ambao ni wadau wakubwa wa elimu hapa Nchi ambapo husapoti serikali katika sekta ya elimu kwa tuoa misaada kwa wanafuzi.
Dc Serera alisisitiza kwamba asilimia kubwa ya wazazi katika wilaya ya Simanjiro wamekumbwa na tatizo la ukame hali iliyopelekea kukosa kipato na hata kumudu michango ya kugharamia chakula mashuleni.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika la maendeleo la Eclat Foundation, Peter Ole Toima alisema kwamba kutokana na ukame wananchi wengi wa maeneo ya wafugaji wamepitia kipindi kigumu hususani kupoteza mifugo mingi kutokana na kukosa malisho."Shirika la Eclat Foubdatiin limeona changamoto hiyo na kuchukua hatua ya kuwashika mkono kwa kuwapatia wanafunzi vyakula kwa lengo la kuongeza mahudhurio ya wanafunzi shuleni kwa kufanya hivyo pia kutasaidia kuongeza kiwango cha ufaulu na Taifa kuoa wasomi wengi katika nyanja mbali mbali, Pia tutakuwa tumewasaidia wazazi katika utoaji wa michango ya chakula mashuleni maana wengi wetu wamekabiliwa mukame na kupoteza mifugo yao mingi kutokana na janga hili la ukame” alisema Ole Toima.
Hata hivyo chakula hicho kinataraji kuwasaidia wanafunzi katika kipindi cha miezi mitatu nachukula kilicho tolewa ni mahindi na maharage ambapo shirika hilo la Eclat Foundation limekabidhi katika shule tatu za msingi na moja ya sekondari wilayani Simanjiro.
Comments
Post a Comment