PINGO's YAZINDUA RIPOTI MPYA ITAKAYO SAIDIA JAMII ZA KIFUGAJI NCHINI KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI.
Na Lucas Myovela.
Ripoti hiyo mpya ya utafiti imebainisha baadhi ya mbinu za asili ambazo zimesaidia jamii za Wamasai kusalia kustahimili mabadiliko ya hali ya hewa.
Na Lucas Myovela_ Arusha.
Matokeo hayo yamechapishwa na Jukwaa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali ya Wafugaji (PINGO's FORUM) yametaja muingiliano wa wafugaji na Habari kuwa ni baadhi ya mambo ambayo yamewafanya wafugaji kukabiliana na adha hiyo. Mabadiliko ya tabianchi maana hupata taarifa mapema

"Wafugaji walionyesha kuwa mabadiliko ya binadamu ni muhimu na kwamba ilikuwa ni aina ya mkakati wa kukabiliana na hali mbaya ya hewa kama vile uoto mdogo wakati wa kiangazi," alisema Dkt Chengula.

"Ni Wamasai tu wa Tanzania na Waturkana kutoka nchini Kenya ambao wanaweza kustahimili hali mbaya kama hii," alisema Dkt Chengula.



"Wamasai walitumia kitoweo kutoka kwa vipande vya gome, mizizi au majani kama dawa," alisema Bw Masaza
Kulingana na Dk Masaza, jamii za wafugaji pia zilitumia Taarifa kama mkakati muhimu wa kuendelea kuwa wastahimilivu katika hali mbaya ya hewa.
Ingawa shughuli kuu ya kiuchumi ya Wamasai ni ufugaji, ripoti inapendekeza kwamba baadhi walilazimishwa kutegemeza riziki zao kwa kilimo cha mazao.
"Wafugaji wengi sasa wanajishughulisha na shughuli nyingine kama vile Kilimo," aliongeza Dk Masaza.
Karibu Motive Media Tz katika kurasa zetu katika mitandao ya kijamii kwa ajili ya taarifa mbali mbali pia wasilia nasi kupitia 0685 858 035 whatsap.
Comments
Post a Comment