YAKA BARIKI JUMA LAKO KATIKA KAZI.
Uje Roho Mtakatifu, tuangaze toka mbingu, Roho zetu kwa mwangao
Uje Baba wa maskini, uje mtoa wa vipaji, Uje mwanga wa mioyo
Ee Mfariji mwema sana, ee rafiki mwanana, Ewe raha mustarehe
Kwenye kazi u pumziko, kwenye joto, burudiko, U mfutaji wa machozi
Ewe mwanga wenye heri, uwajaze waamini, Neema yako mioyoni
Bila nguvu yako wewe, mwanadamu hana kitu, Kwake yote yana kosa
Osha machafuko yetu, panyeshee pakavu petu, Na kuponya majeraha
Ulegeze ukaidi, washa moto wa uadili, Nyoosha upotevu wote
Wape waumini wako, wenye tumaini kwako, Paji zako zote saba
Wape tuzo ya fadhila, wape mwisho bila hila, Wape heri ya milele
Amina aleluya, amina aleluya, Amina aleluya.
Comments
Post a Comment