WASICHANA NA WANAWAKE 7000 KUNUFAIKA

 NI SHILINGI BILIONI 45 KUWANUFAISHA WATOTO WA KIKE KUTOKA WILAYA 12 NCHINI KATIKA MRADI WA UZESHAJI UJUZI ( ESP ).

Na Lucas Myovela Arusha.


Shilingi Bilioni 45 kitatumika  kuwanufaisha watoto wa kike na wanawake zaidi ya 7000 kutoka wilaya 12 za nchini Tanzania kupitia mradi wa uwezeshaji ujuzi (ESP) programu hiyo itachukua takribani kipindi cha miaka saba ( 7 ) hadi kukamilika (2021-2028).


Mradi huo unatekelezwa na Muungano wa vyuo na Taasisi za ufundi Canada (CICan) kwa ushirikiano wa karibu na wizara ya elimu,sayansi na teknolojia Tanzania (MOEST)kupitia idara ya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (DTVET)unaofadhiliwa na serikali ya Canada.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha leo katika warsha ya siku nne ya muelekeo wa ubia kwa ajili ya mpango huo,Mshauri wa mradi wa uwezeshaji kupitia ujuzi (ESP) ,Dokta Alice Mumbi amesema kuwa,mradi huo utaimarisha njia mbadala za elimu,Ajira,kijiajiri na ujasiriamali kwa wanawake na wasichana .


Dokta Mumbi amesema kuwa,mradi huo utafanya kazi na vyuo vya maendeleo ya wananchi (FDCs ) na asasi za kijamii (CBOs) katika jamii 12 nchini Tanzania ,na unalenga kuongeza viwango vya ushiriki kati ya wanawake na wasichana katika programu za mafunzo ya ujuzi na kuboresha upatikanaji wa mafunzo ya biashara ,ujuzi,jinsia na haki za binadamu katika jamii zao.


Aidha amesema kuwa,mradi huo utapanua fursa katika sekta rasmi na zisizo rasmi kupitia usaidizi baada ya mafunzo ili kuingia kwenye ajira au kujiajiri. 


Aidha amesema kuwa mradi huo utafanya kazi na vyuo vya maendeleo ya wananchi 12 vilivyochaguliwa pamoja na asasi za kijamii 12 zilizochanguliwa kwa kuanzisha mtandao wa timu za jinsia na washauri wa kike,kushirikisha jamii katika shughuli za kukuza uelewa wa kijinsia juu ya faida za elimu kwa wanawake na uwezeshaji wa kiuchumi na kutoa mafunzo endelevu kwa washirika hao ya kujenga uwezo katika usawa wa kijinsia ,haki za binadamu,mbinu za ufundishaji na mafunzo ya watu wazima.


Kwa upande wake Katibu Mkuu wa wizara ya elimu,sayansi na teknolojia,Francis Michael amesema kuwa wizara hiyo ni wizara muhimu katika utekelezaji wa mpango kazi wa Taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto nchini Tanzania hasa kwa kuwawezesha wanawake kufuata fursa za kiuchumi na kijamii,kuendeleza mazingira wazushi kwa mahusiano ya usawa wa kijinsia na kwa kusaidia nafasi salama kwa wanawake katika jumuiya zao.


Naye Mkuu wa uendeshaji na Mshauri (maendeleo )masuala ya kimataifa Canada amesema kuwa,Bronwyn Cruden Canada inajivunia kuunga mkono ukuaji wa mpango mpya wa mwitikio wa kijinsia nchini Tanzania kupitia mpango wa uwezeshaji kupitia ujuzi. 

Amesema kuwa, ESP inatoa fursa kwa Canada kuendeleza uwekezaji wake mwingine katika maeneo ya utekelezaji ya elimu,usawa wa kijinsia, haki za binadamu,na ukuaji wa uchumi ambao unafanya kazi kwa kika mtu.


Canada imekuwa mshirika wa muda mrefu katika sekta ya elimu ya Tanzania ,msaada baina ya nchi mbili kimsingi unalenga katika kuboresha ubora na umuhimu wa ufundishaji katika shule za msingi,sekondari, na vituo vya mafunzo ya ufundi na ufundi hasa ujuzi na elimu na mafunzo ya ufundi na ufundi (TVET) ni muhimu katika kupunguza ukosefu wa ajira,ukosefu wa usawa na umaskini na kukuza ukuaji wa uchumi na maendeleo”alieleza.


Kwa upande wake Makamu wa Rais ,kimataifa ,vyuo na Taasisi Canada ,Alain Roy amesema kuwa,vyuo na taasisi Canada inajivunia kupewa fursa na wizara ya elimu, sayansi na Teknolojia na masuala ya kimataifa ya Canada kufanya programu hiyo kwa washirika wa FDCs na AZAKIs .

Comments