KIPANGA AMTAKA MKANDARASI KUONGEZA KASI KATIKA MRADI WA UJENZI WA MAABARA YA TAEC KANDA YA MASHARIKI

Na Lucas Myovela

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Omari Kipanga amemtaka Mkandarasi wa kampuni ya Group Six International Limited kuongeza kasi ya ujenzi katika mradi wa Maabara, Ofisi na Mtambo wa Kinururisho Jumuishi -Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Kanda ya Mashariki.


Mhe. Kipanga ametoa agizo hilo jijini Dar es Salaam alipofanya ziara kukagua mradi huo wa Maabara, Ofisi na Mtambo wa Kinururisho Jumuishi -Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Kanda ya Mashariki.

Amesema pamoja na ubora wa kazi inayoendelea ni vizuri kazi hiyo ikakamilika kwa wakati ili majengo hayo yaweze kutumika kwa kazi zilizokusudiwa.


"Ninawapongeze Tume kwa usimamizi mzuri wa kazi ninaona kazi nzuri, nasisitiza kuongeza kasi ili kazi ikamilike kwa wakati,"amesema Mhe. Kipanga.


Mradi wa ujenzi wa Maabara, Ofisi na Mtambo wa Kinururisho Jumuishi -Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Kanda ya Mashariki unatekelezwa na Mkandarasi Group Six International Ldt kwa gharama ya Shilingi Bilioni 7.9 katika eneo la Mbezi Msakuzi, Dar es Salaam.


Comments