TUMIENI MAONYESHO YA NANENANE KUJIFUNZA NJIA BORA ZA KIUCHUMI.

MAONYESHO YA NANENANE KANDA YA KASKAZINI YAFUNGULIWA YAANZA KWA KIWANGO CHA JUU.

Na Lucas Myovela - Arusha.

Wakulima,Wafugaji na Wavuvi Kanda ya Kaskazini wametakiwa kuyatumia vyema maonyesho ya Kilimo ya Nanenane katika viwanja wa Themi Mkoani Arusha ili kuweza kujiinua kiuchumi kwani maonyesho hayo yana fursa kubwa kwao.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Nurdin Babu wakati akifungua maonyesho hayo ya 30 katika viwanja hivyo baada ya kutembelea mabanda ya maonyesho na kujionea zana za kilimo,mbegu Bora na za kisasa,Madume ya ng'ombe wa kisasa na ufugaji Bora na wa kisasa wa Samaki.


Alisema serikali imejenga mazingira mazuri ya kuboresha sekta ya kilimo.mifugo Na uvuvi hivyo Basi wahusika katika sekta hiyo wanapswa kuiunga mkono Serikali kwa kujitoa ili waweze kuinua uchumi wa mtu mmoja ama ushirika.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Kilimanjaro alisema maonyesho ya Nanenane ni nguzo kuu ya uchumi Kwa Kanda ya Kaskazini hivyo wakulima,Wafugaji na Wavuvi Kanda hiyo wanapswa kuchangamkia fura hiyo ili waweze kujikwamua kiuchumi kwani sekta hiyo Serikali imewekeza mamilioni ya fedha Kwa ajili yao.


Alisema asilimia 90 ya watanzania wanategemea sekta hiyo na ndio maana Serikali imewekeza mamilioni ya fedha na itasikitisha kuona Wananchi wanakaa kimya bila kuchangamkia mamilioni hayo Kwa ajili ya kujiendeleza Kwa lengo la kujikomboa kiuchumi.


Babu amewahimiza wawekezaji kuuza zana za kilimo kwa bei rafiki ili zana hizo ziweze kuwasaidia wakulima katika kujikomboa kiuchumi kwani Bei alizoona katika mabanda ziko juu na haamini kama zinaweza kununuliwa na wakulima wadogo wadogo wadogo ambao Ni wengi katika Kanda hii Na nchi kwa ujumla.


Alisema wakulima wadogo ni wengi hapa nchi Na ndio nguzo ya nchi hivyo nao wanapaswa kusaidiwa ikiwa ni pamoja na kuuziwa zana za kilimo Kwa Bei Rafiki ili watumie katika Kilimo kuliko hivi Sasa wanatumia jembe la mkono.

Mkuu huyo wa Mkoa aliwahimiza wakulima kulima kisasa ikiwa ni pamoja na kutumia mbegu za kisasa zenye kuhimili nyakati zote za majira ya mvua na kiangazi ili ziweze kuota Kwa wakati muafa Kwa kutumia mbolea ama kutotumia mbolea.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maonyesho ya Nanenane Mkoani Arusha ambaye pia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha (RAS),Missaile Mussa alisema kuwa maonyesho hayo mwaka huu yameshirikisha viongozi wote wa Serikali na vyama vya ushirika katika Kanda ya Kaskazini Na maandalizi yalianza aprill 24 mwaka huu.


Mussa alisema wakuu wa Mikoa ya Arusha,Kilimanjaro na Manyara,Wakuu wa Wilaya,Wakurugenzi na wenyeviti wa Halmashauri wote walishirikishwa katika kuhimiza wakulima, Wafugaji na Wavuvi Kanda hiyo kushiriki maonyesho hayo lengo likiwa kuwainua kiuchumi.












Aidha katika hatua nyingine katika maonyesho hayo ya nanenane kwa mwaka huu 2024 yaliyoweza kuhudhuliwa na wataalam mbalimbali wakiwemo watoa tiba zitokanazo na mimea na wameweza kufunguka juu ya manufaa ya maonyesho hayo.

Motive Media imweza kuongea na mtaalam wa tiba asili anae tengeneza dawa zitokanazo na mimea na ameweza kufunguka juu ya fahari kubwa ya uwepo wa kilimo na utunzaji wa mazingira hasa katika uhifadhi wa mimea asili hapa nchini.

Mtaalamu wa Dawa Asili, Kinga na Tiba hapa nchini dokta KAZOBA ametia timu katika viwanja vya Nane Nane Njiro, Arusha ikiwa ni utaratibu wake wa kuhudumia afya za watu kwa kutumia miti shamba na mimea ya asili.



Dokta Kazoba amewataka wananchi kuweza kutumia dawa za asili kama tiba mbadala maana zinauwezo mkubwa wa wa kupambana na magonjwa sugu hasa magonjwa yasiyo ambukiza ambayo kwasasa yanatishia ulimwengu.


Akitoa elimu kwa wananchi katika maonesho hayo ya nane nane wakati wa ufunguzi wa maonesho ya 30 ya nanenane kanda ya kaskazini Dokta. Kazoba amejinasibu kuwa dawa zake zimefanyiwa utafiti wa hali ya juu na zinauwezo mkubwa wa  kupambana na kutibu magonjwa mbalimbali likiwepo tatizo  la upungufu wa nguvu za kiume.



Amesema kwasasa dunia inasumbuliwa na magonjwa mengi kama vile,kisukari, upungufu wa nguvu za kiume unaotokana na ulaji wa vyakula, magonjwa ya moyo, miguu, ukosefu wa uzazi unatokana na utumiaji wa madawa ya kisasa kwa wanawake, n.k.



"Niwahakikishie watanzania wenzangu nimejikita katika utoaji tiba kwa njia ya asili iliyo boreshwa na dawa zetu zinatoa majibu ya haraka niwaombe wananchi waliyopo Arusha na mikoa jirani wafike katika viwanja hivi vya nanenane njiro nitakuwa hapa kwa siku zote za maonyesho na kuwapa dawa za asili zitakazo tibu maradhi kulingana na maradhi ya mtu".Dokta Kazoba.
 

Comments