ENG. HAMSINI AWATAKA WATUMISHI KUHAKIKISHA MIRADI YA SERIKALI INAKAMILIKA KWA WAKATI NA KWA UBORA UNAOTAKIWA ILI JAMII INUFAIKE NA HUDUMA ZA SERIKALI.

WATUMISHI WAMSHUKURU ENG. HAMSINI KWA KUWAKUTANISHA PAMOJA KWA MAENDELEO YA JIJI LA TANGA.

Na Lucas Myovela - Tanga.

Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Mhandisi Juma Hamsini amewataka watumishi wote wa halmashauri ya Jiji hilo la Tanga pamoja na wakuu wote wa idara kuhakikisha miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inakamilika kwa wakati ma kwaubora unaotakiwa ili wananchi wa Jiji hilo waweze kunufaika na huduma za serikali.

Mhandisi Hamsini ameyasema hayo mapema leo Septemba 18, 2024 katika kikao kazi maalu cha Menejimenti ya Halmashauri hiyo (CMT) pamoja na  Watendaji wa Kata, Waganga Wafawidhi, Wakuu wa Shule za sekondari na Msingi.

Kikao hicho kilikuwa na lengo la kukumbushama uwajibikazi kazini na kufanya kazi kwa weredi kwa mujibu wa viapo vya kazi kwa kila mtumishi,kufahamiana, kuweka mikakati ya pamoja, na kutatua changamoto za kiutendaji katika Jiji hilo.

"Niwakumbushe watumishi wenzangu kila mmoja wetu akifanya kazi kwa uadilifu na uhaminifu ni imani yangu kila mwanchi itafuahia huduma inayotolewa na serikali, Maana tayari serikali ya Dkt. Samia imeshaonyesha njia kwa kutoa fedha za maendeleo kwaajili ya wananchi wake". Amesema Eng. Hamsini.

"Ndg. Viongozi wenzangu  niwaombe sana hasa wakuu wa idara  na kila mmoja kwa nafasi yake ya utumishi kuhakikisha miradi hii tuliyopewa inakamilika kwa wakati, na kwa kuzingatia ubora, ili jamii inufaike na mipango ya Serikali ya kuwasogezea huduma karibu". Amesisitiza Hamsini. 

Aidha Mhandisi Hamsini  amehimiza uwajibikaji kwa watumishi, na utoaji wa huduma bora kwa jamii kwa kila mtumishi wa halmashauri hiyo kwa maslahi mapana ya Serikali na Taifa kwa ujumla maana Serikali imewaamini wao na kuwapa nafasi za kuwahudumia watanzania.

Aidha katika hatua nyingine watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga wamempongeza Mhandisi Hamsini kwa kuwaleta pamoja na kukumbushana majukumu ya kiutendaji na kuahidi wataenda kutenda kazi kwa weledi na bidii kwa maslahi mapana ya serikali.


Pia watumishi hao wamemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini Eng. Hamsini na kumpa jiji la Tanga na kueleza kuwa kwasasa wanaiona Tanga Mpya ambayo ilikuwa ndito ya kila mtumishi kuona jiji hilo linakuwa mfano wa kuigwa hapa nchini.


Ikumbukwe Eng. Hamsini kwasasa ni Mkurugenzi wa Tanga na hiki ni kikao chake cha kwqnza na watumishi wote wa Halmashaui hiyo akitokea Jiji la Arusha baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanya mabadiliko ya viongozi mbalimbali mwezi Agosti 2024.







Comments