KAMPENI MAALUMU YA SITAPELIKI YAZINDULIWA, NAMBA MAALUMU YA HUDUMA KWA WATEJA NI HII.

 SASA NI MAKAMPUNI YOTE YA SIMU KUTUMIA NAMBA 100 KUWASILIANA NA WATEJA WAO.Na Lucas Myovela - Arusha.

Arusha: Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa amezindua kampeni ya "Sitapeliki" itakayowasiliana na mteja au watoa huduma kwa namba 100 pekee kutoka kampunzi za simu zilizopo nchini.

Kampeni hiyo ya "Sitapeliki "imezinduliwa jana Jiji ni Arusha na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari , Jerry Silaa ili kudhibiti wizi mtandaoni kupitia simu za mikononi kwa wananchi wanaopiga matapeli kupitia namba zisizotambulika ambayo ni 100 pekee kwaajili ya kuwasiliana.

Amesema watoa huduma wa kampuni zote za simu wanawasiliana na wateja wait kupitia namba ya 100 pekee epuka utapeli na ulaghai mtandaoni, kampuni za simu toeni elimu kwa wananchi ili was utapeliwe"


"kampeni hii ya pamoja ni mkakati wa serikali na kampuni za simu kutoa elimu kwa umma kupitia jumbe mbalimbali zitakazotumwa kwa wamiliki wa simu kupitia kampuni mbalimbali ili kuepuka utapeli kutoka kwa matapeli wanaorubuni wananchi kupitia simu za kiganjani". Mesema Silaa


Aidha Silaa ameeleza kuwa kikao hicho cha wadau wa mawasiliano ya simu kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imelenga kuhakikisha kampeni hiyo ya sitapeliki inalengo la kutoa elimu kwa jamii katika kushughulikia utapeli huo mtandaoni huku akinukuu jumbe chache zitakazotumwa kwa wananchi kupitia simu zao


"Ni vema kulinda taarifa zako kwa kutumia nywila sahihi na tofauti kwa kila akaunti ikiwemo namba, Alamance, herufi kubwa na ndogo, usifuate maelekezo au kutoa neno la siri(nywila) kwa mtu yoyote, linda taarifa zako kwakuepuka kubofya viungajlnishi usizovifahamu, uhakiki wa namba ya simu kupitia*106# kisha chagua kuona namba zilizosajiliwa na NIDA". Ameeleza Silaa.


Pia ujumbe mwingine ni kukumbushwa mtoa huduma atawasiliana na wataje wake kupitia namba 100 pekee na kama si namba 100 usitoe taarifa zako huku ujumbe wa sita ni usiruhusu utapeli au ulaghai wa simu au ulaghai wa simu. 


Silaa amesisitiza kuwa kwa sasa serikali haijapokea taarifa za udukuzi wa mawasiliano kutoka kwa wateja ikiwemo kutumia mtandao kwa usahihi huku akisisitiza kampuni za simu kutoa elimu kwa wateja huku jeshi la polisi na TCRA waendelee kudhibiti matukio ya kiulaghai kupitia mitandao ya simu ikiwemo kuathiri mifumo ya kifedha kupitia kidigiti.

Comments