AAPA KUWANYOOSHA MATAPELI KUELEKEA UCHUMI WA KIMTANDAO.
ASEMA MPAKA SASA LINE ZA SIMU NI MILIONI 86.
Na Lucas Myovela - Arusha.

"Niwaombe wanahabari wote nchini, wasanii na watu wote mashuhuri tuungane kwa pamoja katik kmpeni hii ya "sitapeliki" ili kuweza kumaliza wimbi la utapeli katika nchi yetu nina imani kila mtanzania akiwa mlinzi wa simu yake na kuto kutoa siri za akaunti yake tutaweza kupiga hatua kubwa". Amesema Silaa.

"Niwaombe sana watanzania kuweka namba za siri ambazo hagatani ili kuepusha kuibiwa fedha zao mtandaoni, Pia wasiwe wepesi kutoa taarifa pindi wanapo pigiwa simu na watu wasiyo wajua kwasasa ukipigiwa aimu mtu akajitambulisha ametoka mtandao furani na namba ya kaida mripo haraka sana ili aweze kufuatiliwa". Ameongeza Silaa.
Aidha katika hatua nyingine Waziri Silaa ameelezea mwenendo na ukuaji wa mawasiliano hapa nchini ambapo kwa sasa nchi nzima imweza kugikiwa na mawasiliano na uboeshaji wa mkongo wa taifa ukielekea kukamilika na kupunguza changamoto kadhaa za kimtandao.
"Kwasa kwa Tanzania kuna line za simu milioni themanini na sita na laki nane ( 86,800,000) ambazo zinatumika hii inaonyesha mashirikiano mazuri ya serikali na taasisi za mawasiliano". Amesema Silaa.
Ameeleza kuwa mbali na kuwa na changamoto uboreshaji bado unaendelea kwa kushirikiana na wadau wote wa mawasiliano pamoja na vyombo mbalimbali vya kimamlaka ili kuweza kuifikia dira ya mafanikio.
Kampeni hiyo ya "Sitapeliki " imezinduliwa jana Jiji ni Arusha na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari , Jerry Silaa ili kudhibiti wizi mtandaoni kupitia simu za mikononi kwa wananchi wanaopiga matapeli kupitia namba zisizotambulika
Kwasasa namba zitakazo tumika kwa nchi nchi nzima kuwasiliana na mteja kutoka kwa mtoa huduma ni 100 pekee na namba ya kuripoti tukio la kupigiwa simu na matapeli ni 15040 na namba ya kuangali namba yako ya NIDA imesajili line ngapi ni *106#.
Comments
Post a Comment