🔻DKT. BITEKO AAGIZA KUWEKWA MFUMO WA UMEME WA DHARURA KATIKA KITUO CHA KUSUKUMA MAJI NAMBA 5 CHEKERENI JIJINI ARUSHA.
Amesema katika kilele cha maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano ambapo amewahimiza Watanzania kukumbuka kuwa kuwa Mwl. Julius Nyerere na Hayati Mzee Abeid Amani Karume waliunganisha Tanganyika na Zanzibar katika misingi ya umoja, amani, ushirikiano na kuheshimiana hivyo, muhimu kuendeleza misingi hiyo ili kuenzi Muungano.
Dkt. Biteko amesema hayo leo Aprili 26, 2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Soko la Kilombero, Wilaya ya Arusha Mjini, Mkoa wa Arusha.
"Arusha mfanye kazi kwa kushirikiana, muijenge Arusha yenu mkumbuke kwenye nafasi zetu za uongozi mjue kesho hamtakuwepo mtaondoka, kila mahala ulipo acha alama njema itakayo kumbukwa na wengine". Amesema Dkt Biteko.
"Sisi tuliopo leo tutakumbukwa kwa lipi, iwe changamoto tunapokumbuka miaka 61 ya Muungano tujue ni alama gani tutaacha kwa watoto wetu," Ameongeza Dkt. Biteko.

"Hicho ndicho kiwe kipimo na viongozi tusitumie tofauti zetu kutafuta kura, usiende kanisani au msikitini kwako kutumia uhalali watofauti zetu kutafuta kura asitokee yeyote kufanya hivyo tuuenzi Muungano na Rais Samia ameapa kuulinda Muungano huu kwa wivu mkubwa," amesema Dkt. Biteko.
Dkt. Biteko amebainisha Watanzania wasiruhusu Taifa kugawanyika kwa sababu yoyote ile wakumbuke kuwa
kama hakuna amani hakuna biashara wala maendeleo yanayoweza kufanyika.
NAIBU WAZIRI MKUU AKAGUA KITUO CHA KUSUKUMA MAJI SAFI ARUSHA.

Katika ziara hiyo, Dkt. Biteko ameagiza Kuwekwa mfumo wa umeme wa dharura (backup) katika kituo hicho,Kuimarishwa kwa juhudi za kudhibiti upotevu mkubwa wa maji na Kuboresha huduma za maji kwa wananchi.
Aidha, Dkt. Biteko amekagua maendeleo ya miundombinu ya mradi huo na kupanda mti wa kumbukumbu katika eneo hilo.
Comments
Post a Comment