RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA MADARAJA MAWILI MUHIMU YANAYO UNGANISHA MIKOA YA KASKAZINI. UJENZI KUKAMILIKA JULAI 2, 2025.
RC MAKONDA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA MRADI WA MADARAJA YA KING’ORI BARABARA YA ARUSHA – MOSHI.
Na Lucas Myovela -Arusha.

Aidha, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuhakikisha miundombinu ya barabara nchini inaboreshwa na kuwa salama wakati wote – iwe ni kipindi cha mvua au kiangazi pamoja na kuipongeza Wizara ya Ujenzi na taasisi husika kwa kutekeleza kwa ufanisi maelekezo ya Mhe. Rais.
Hata hivyo, mesisitiza umuhimu wa watumiaji wa barabara kufuata sheria na taratibu za usalama barabarani ili miundombinu hii iweze kudumu kwa muda mrefu, hasa ikizingatiwa kuwa barabara hii inapita magari makubwa ya mizigo na pia hutumiwa na watalii wengi wanaotembelea maeneo ya kitalii ya Kaskazini mwa Tanzania.
Mradi huo unatekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia kwa gharama ya shilingi bilioni 4.6 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Julai 2, 2025.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Eng. Martin Bouchard kamala kutoka kampuni ya Abemulo contractors co Ltd wanaotekeleza mradi huo ameeleza kuwa mpaka sasa mradi unaendelea salama mbali na changamoto za mvua kuendelea kunyesha wanajitahidi kwa kila hali ili kumaliza mrasi huo ndani ya wakati.
"Mvua zisipo kuwa kubwa ni imani yangu mradi huu tutamaliza mdani ya mkataba ila kama mvua zitazidi itabidi tufanye kadri tuwezavyo na itabidi tuombe ongezeko la muda ili kufanya kazi kwa ufanisi na ubora wenyeviwango vikubwa". Amesma Eng. Kamala.
Comments
Post a Comment