KAMA NI MWANAHISA CRDB HII UMETOBOA KWA GAWIO NONO.
Na Lucas Myovela - ARUSHA.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya CRDB, Dkt. Ally Laay, ameeleza kuwa kutokana na faida hiyo bodi ya wakurugenzi imependekeza gawio la shilingi 65 kwa kila hisa ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 30, kulinganisha na gawio la mwaka jana 2024 ambalo lilikuwa ni shilingi 50 kwa hisa.
"Kutokana na faida hiyo, Mkutano Mkuu wa 30 wa Wanahisa wa benki uliopangwa kufanyika Jumamosi mei 17, 2025 katika kituo cha kimataifa cha mikutano cha AICC jijini Arusha pamoja na mambo mengine, unatarajiwa kupitisha pendekeo hilo la ongezeko la gawio kwa hisa linalotokana na benki kuendelea kupata matokeo mazuri sokoni". Ameongeza Dkt. Laay.

"Kupitia njia ya mtandaoni wanahisa wataweza kujiunga kuanzia saa 2:00 asubuhi kupitia tovuti ya benki hiyo au mfumo wa benki hiyo waliopakua katika simu au kompyuta zao tayari tumeweka mwongozo wa jinsi ya kushiriki mkutano mkuu kwa njia ya mtandao kupitia tovuti yetu, mitandao yetu ya kijamii, pia maelekezo yametumwa kwa ujumbe mfupi kwa wanahisa". Amesema Dkt. Laay.

Nsekela ameeleza mkakati wa kuendelea kufungua matawi ya benki hiyo nje ya nchi ambapo kwasasa wamefanikiwa kufungua tawi katika nchi ya Burundi ma tawi hilo linalofanya vizuri zaidi na kuifanya kuwa benki kinara katika nchi hiyo.
"Benki yetu imefanikiwa kuingia nchi ya DR Kongo na Tayari tumefungua matawi katika miji ya Kinsasa na Lubumbashi ambayo yanaendelea vizuri, mpango wetu mwingine ni kufungua tawi katika nchi ya Dubai na tayari tumeshapata kibali na mchakato wa kupata eneo la kufungua tawi la CRDB unaendelea na mipango mikubwa ni kufungua matawi katika nchi mbalimbali za Afrika unaendelea". Amesema Nsekela."Thamani hisa ya benki yetu imeongezeka baada ya kuwepo kwa hamasa kubwa kwa ununuzi wa hisa kwa mtu mmoja mmoja hii ni kutokana na maboresho ya miundo mbinu, ubunifu mkubwa na kuongezeka kwa mapato na kubana matumizi kitu ambacho kimetugikisha katika mafanikio haya ambayo wanahisa wanaenda kunufaika nayo". Ameongeza Nsekela.
Aidha Nsekela amewataka wanahisa wote wa Benki ya CRDB kujitokeza kwa wingi kwa kuwa ushiriki wao utawezesha Bodi na Menejimenti kupata maoni yao ya namna bora ya kuboresha huduma za kibenki na kuweka mawazo ya pamoja na muelekeo wa benki hiyo kwa ukuaji kimapato na huduma bora kwa wateja.
Comments
Post a Comment