CATHELINE MAGIGE NA ZAITUNI SWAI WAANGUKIA USO KWENYE ZEGE ZITO LA WAJUMBE.
Majina mapya ya wagombea wa nafasi hiyo yameonekana kushika kasi kwa wajumbe hao kitu ambacho kimebadilisha upepo na kuwaacha midomo wazi wabunge waliyo kuwa wanatetea nafasi zao za ubunge.
Uchaguzi huo ulifanyika na kusimamiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Kenani Laban Kihongosi na kuhudhuliwa na viongizi mbalimbali wa chama pamoja na wajumbe husika.
Akisoma matokeo hayo mara baada ya wajumbe kupiga kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Kenani Kihongosi alisema kuwa wajumbe waliyo hudhudhilia Mkutano huo ni 1261 na wote walipaga kura.
"Idadi ya Kura zilizo pigwa ni 1252, Akidi ya wapiga kura 1661, Idadi ya kura zilizo haribika ni 7, Idadi ya kura halali ni 1245". Alisema Kihongosi.
Akitangaza matokeo hayo Kihogosi alisema kuwa Lilian Joseph Badi amepata kura 9, Martha Martin Amo amepata kura 50, Navoi Mollel amepata kura 95, Zaytun Seif Swai amepata kura 141, Dkt. Asanterabi Ngoyai Lowassa amepata kura 196, Catheline Valentine Magige amepata kura 213, Chiku Athuman Issa amepata kura 775 na Martha Gido Kivunge amepata kura 1004.
USHINDI WA CHIKU NA MARTHA.
Chiku Issa ni moja ya watumishi makini waliyojikita katika maswala ya utawala wa fedha, uchumi na siasa kitu ambacho kwasasa kinaonekana kuzaa matunda katika taia la Tanzania.
Chiku Athuman Issa ametumikia taasisi ya fedha ya Benki ya CRDB kama meneja wa kanda ya kaskazini na kwasasa ni Mjumbe wa kamati ya Uchumi, Mpango, Fedha UWT Taifa, Mjumbe wa Mkutano UWT Taifa, Mjumbe wa kamati ya Utekelezaji wilaya Arusha jiji.
Hadi sasa matamanio ya wanachama wa chama cha mapinduzi ni majina haya mapya yaweze kurudi ili waweze kuwatumikia wana UWT Mkoa wa Arusha.
Kufuatia kanuni za chama mara baada wajumbe kupiga kura majina hayo huchujwa (mchujo wa ndani) ambao utakaoamua nani kati ya wale waliochaguliwa ndio atateuliwa rasmi kufuatia uwiano wa viti maalum wa chama na hupangwakulingana na uwiano wa kura zilizopatikana na chama katika uchaguzi mkuu.
ANGUKO LA CATHELINE MAGIGE NA ZAYTUNI SWAI.
Inaelezwa kuwa kwa kipindi kirefu wawili hao walikuwa na magenge ya kiasiasa kitu ambacho kiliwachanya wanachama na kutofurahia mwenendo wa siasa zao kwa maslahi mapana ya chama.
Bado hadi sasa inatajwa kuwa kila mmoja alifanya vizuri kwa upande wake kwa UWT na kujiimarisha ili asije piteza nafasi yake ila wajumbe wamefika ukomo wa migorogoro ndani ya chama na kutaka kuijenga CCM moja iliyo imara, madhubuti na yenye kutatua changamoto za wananchi.
Je, unahisi ni haya tu yanayosemwa na wana UWT au kunamengine ambayo yamewapelekea anguko hili kubwa la aibu ndani ya chama huku ikieleza Cathereen Magige ni mzoefu na mekaa kwa zaidi ya miaka 18 bungeni au ndiyo kil mtu aonje keki ya Taifa au ndiyo kuchanika kwa jamvi sio mwisho wa maongezi.
Comments
Post a Comment