KIHONGOSI ATAKA AMANANI NA MSHIKAMANO, AMUAGIZA MKURUGENZI KUTOA ELIMU YA MIKOPO.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kenani Kihongosi amewahimiza wafanyakazi wa saloon na waajiri kulinda tunu ya Taifa pamoja na amani iliyopo nchini na kuwataka kufanya kazi kwa kanuni na sheria za nchi.Rc Kihongosi ameyasema hayo mapema leo alipokuwa akiongea na wamiliki, wafanyakazi wa saloon katika Jiji hilo kwa lengo la kubaini changamoto zao na kutafutia utatuzi sahihi ili kuondoa migogoro inayoweza kujitokeza pamoja na kusisitiza suala la usafi wa maeneo wanayofanyia kazi.
Kihongosi ameeleza kuwa watu wa saluni ni kada nzuri yenye wateja wengi hivyo wanapoona kunahabari tofauti za wateja wao watoe taraifa serikalini ili hatua ziweze kuchukuliwa na kusisitiza kulinda amani kwa kutoa viashiria ambavyo havijakaa sawa.
"Mikopo hii mkiichukua kwa malengo itawasaidia na itasaidia kukuza kipato cha kila mmoja wetu, Niwahakikishie tumejipanga vyema kuhakikisha tunawahudumia na kuwapa elimu ya usimamizi wa fedha ili Arusha yetu iwe imara kiuchimi".Ameeleza Kayombo.




.jpg)




Comments
Post a Comment